Wednesday, 26 July 2017

KAULI YA JOSEPH YONA KUHUSU CHADEMA KUHAMIA CCM

Ni kauli za mwenyekiti wa chama cha mapinduzi tawi la bokorani JOSEPH YONA


Ameyazungumza hayo baadaya ongezeko la madiwani wa chama cha chadema kuhamia ccm

Alisema CHADEMA ni chama ambacho nakijua si chama cha chenye mipango ya kumkomboa mwananchi Si chama chenye democrasia wala uhuru wa kuhoji wala kujieleza wala kukosoa ni chama chenye muundo tofauti na CCM kwani maamuzi yote yanafanywa na watu wachache na ndio maana wengi wanakimbia sababu hakuna uhuru wa kisiasa

Alisema CHADEMA inapaswa kupingwa na wananchi wote wapenda maendeleo wapenda Taifa kwani hawana mapenzi na maendeleo ya TAIFA aliongeza na kusema kuwa ni wakati wa TANZANIA kusonga mbele ni wakati wa TANZANIA kupiga hatua tunapaswa kumuunga mkono  Rais wetu kipenzi mwenye kukesha na kupigania Tanzania mpya ya viwanda

WATANZANIA tuweke tofauti pembeni tulipiganie Taifa JPM ni binadamu kama sisi ana moyo na damu kama hatuta Muunga mkono tutamfanya awe mpweke tufahamu ya kuwa hatuna Rais Mwingine kwa sasa

WAPINZANI tunawapenda sana tunaomba hoja za kulijenga Taifa na kumkomboa Mwananchi wa Tanzania

Serikali tunaiomba iwashughulikie wanasiasa wote wenye kuleta siasa chafu za kuvuruga amani ya nchi bila kujali vyama wanavyo tokea ili kuleta usawa na haki katika taifa.

Alizungumza leo katika ofisi za chama cha mapinduzi Tawi la bokorani lililopo Kata ya Mtoni wilaya Temeke Jijini  Dar es salaam



Joseph yona
Mwenyekiti ccm bokorani

0 comments:

Post a Comment

DataTz Group Tech

DataTz Group Tech
Ni mtandao wa Kuhamasisha,Kuwawezesha Wajasirimali wadogo na wakubwa waweze kupata soko la Bidhaa/Huduma zao kwa Njia ya mtandao wa internet. Tunawatengezea BLOG, WEBSITE, LOGO, PHONE APP, vitabu, mashapisho na kurasa za Facebook, Instagram, Twitter. Wasiliana nasi kwa Email datatz88@gmail.com Simu 0763491136/0714067875/0688496762 Asante na Karibu Sana.